Na Selemani Nambimbi, CMU
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimeendelea kuonesha dhamira yake ya kukuza lugha na fasihi ya Kiswahili kwa kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya miaka 10 ya Tuzo za SAFAL Kiswahili Prize for African Literature, ambazo zimekuwa zikihamasisha waandishi barani Afrika kuandika kwa Kiswahili.
Hafla ya utoaji wa tuzo hizo ilifanyika Julai 24, 2026 katika Ukumbi wa Maktaba Mpya wa UDSM na kuhudhuriwa na wanataaluma, waandishi, wachapishaji, watunga sera na wadau wa fasihi kutoka nchi mbalimbali za Afrika.











